Breaking News

MAMBO YA KUZINGATIA KABLA YA KUINGIA KWENYE UCHUMBA

 

Kutokana na kumheshimu unamkatalia. Mumeo anaporudi unamweleza tukio zima lilivyokuwa, cha ajabu wala hakasiriki, sana sana anakulaumu kwa kumnyima ndugu yake unyumba! Kumbe hizo ni mila zao, lakini wewe ulikuwa hujui kabla, sasa katika hali kama hii utajisikiaje? Lakini ukumbuke kwamba kama ungemchunguza vizuri, ungejua mambo hayo na pengine usingeingia katika ndoa hiyo.

UNAYEMPENDA KWA DHATI

Hii isibaki kuwa hadithi za kufikirika, iwe yakini na moyo wako uzungumze hivyo, kuwa unampenda kwa mapenzi ya dhati! Utajuaje kama unampenda? Sema na moyo wako utakupa ukweli juu ya hilo, usikurupukie mapenzi, usije ukamuona msichana siku moja ukamtamani ukadhani unampenda, utakuwa unapotoka!

Mapenzi huanza moyoni, jiridhishe kwanza ndipo ukubali kumwingiza katika moyo wako. Kumbuka unapoamua kufunga ndoa na mtu ni ahadi ambayo mmeahidiana mbinguni na duniani. Ni ahadi ambayo inapaswa kutenganishwa na kifo tu, sio vinginevyo! Kamwe usifanye majaribio katika mapenzi, mapenzi hayajaribiwi. Kitu cha kuzingatia zaidi katika kipengele hiki ni kwamba, lazima awe anakuvutia zaidi.

Usipomuona kwa siku kadhaa moyo wako unakuwa hauna amani kabisa. Akitokea tu, moyo wako unafurahi na kuona kweli mpenzi unaye. Kuingia katika ndoa na mwenzi ambaye hakuvutii ni hatari maana baadaye unaweza ukajikuta unatamani kutoka nje ya ndoa. Usiruhusu hilo litokee. Jiridhishe kwanza, awe anakuvutia ndipo ufikirie suala la kuwa mchumba wako na baadaye ndoa.

No comments