Breaking News

SMS ZENYE KUNOGESHA MAHABA KILA SIKU

 

Natamani ningekuwa chozi jichoni mwako ambapo ningetelemka na kuishia midomoni mwako, lakini kamwe sitamani uwe chozi jichoni mwangu nitakupoteza kila muda niliapo.
*******
Naweza kuishiwa ujumbe wa kukutumia. Naweza kuishiwa utani pia. Naweza kuishiwa chaji lakini moyo wangu hauwezi kukosa nafasi ya kukuweka.
*******
Unaweza usione kamwe ni kwa kiasi gani ninavyokujali. Unaweza usisikie ni kwa kiasi gani nilivyokushiba, unaweza usihisi namna gani ninavyokukumbuka. Sababu ni moyo wangu tu uliyoyaficha hayo.
******
Furaha yangu kubwa ni kuliona tabasamu lako, kujua uko na furaha, na kuhisi upendo wako. Najua kuwa maisha mara nyingine huwa ni makatili, na hiyo ni sababu niko hapa kukuonyesha kuwa maisha yanaweza kuwa mazuri kama kuna mtu anayekujali.
****
Ningependa siku moja utamani sana kuwa na mimi, na uhangaike sana kunitafuta, ili ujue ni kwa kiasi ninavyotamani kuwa nawe sasa.
****

No comments